• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

Elimu sekondari

Halmashauri ya wilaya ya Ushetu ina shule 18 za sekondari katika Kata 16 zenye kidato cha 1-4, miongoni mwa shule hizi shule moja ya Dakama ina wanafunzi wa kidato 5 & 6 katika Tahasusi za PCM na HGL ambao walianza mwezi Julai, mwaka 2015 baada ya shule hii kupata kibali cha kuwa na wanafunzi wa kidato cha tano (5) na sita (6). Shule hizi zote ni za serikali na Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu haina shule yeyote ya sekondari inayomilikiwa na mtu binafsi au shirika.

Shule zilizopo zina jumla ya wanafunzi 5,590 ambapo wavulana 3078  na wasichana 2512.

Idadi ya walimu katika shule za sekondari.

uwiano wa mwalimu kwa wanafunzi katika shule za sekondari

S/N
Kata
S/N
Jina la shule

Idadi ya wanafunzi
Idadi ya walimu
Uwiano wa Mwalimu: wanafunzi
1
Mpunze
1
Mpunze
396
17
1:23
2
Nyamilangano
2
Kisuke
535
21
1:25
3
Bulungwa
3
Bulungwa
455
19
1:23
4
Chambo
4
Chambo
282
17
1:16
5
Chona
5
Chona
339
11
1:30
6
Ukune
6
Dakama
435
22
1:20

Ukune
7
Ukune
133
13
1:10
7
Idahina
8
Idahina
249
12
1:20
8
Ushetu
9
Mweli
252
16
1:15

Ushetu
10
Ushetu
230
17
1:13
9
Ulewe
11
Ulewe
375
12
1:31
10
Ulowa
12
Ulowa
590
16
1:36
11
Uyogo
13
Uyogo
261
14
1:18
12
Kinamapula
14
Kinamapula
356
16
1:22
13
Igwamanoni
15
Igwamanoni Sekondari
280
16
1:18
14
Igunda
16
Igunda
142
8
1:18
15
Nyankende
17
Nyankende
132
11
1:12
16
Sabasabini
18
Sabasabini
148
8
1:18
17
Ubagwe

-



18
Kisuke

-



19
Mapamba

-



20
Bukomela

-




JUMLA
5590
 266
 1:21


Halmashauri ina walimu 266, kama takwimu zinavyoonesha hapo juu, kwa mtizamo wa kawaida walimu waliopo wanaotosheleza mahitaji hususani kwa masomo ya sanaa na lugha. Changamoto kubwa iko upande wa walimu wa sayansi na hisabati ambapo hadi sasa upo upungufu wa walimu 100.
Maendeleo ya Taaluma
Shule za sekondari katika halmashauri ya wilaya ya Ushetu zimekuwa zikifanya vizuri mwaka hadi mwaka, mfano jumla ya wanafunzi 124 waliomaliza kidato cha nne mwaka 2014 walichaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha 5 katika shule mbalimbali za serikali na wanafunzi wengine walijiunga na vyuo mbalimbali katika ngazi za astashahada na stashahada na asilimia ya ufaulu kiwilaya ilikuwa 79.83.
 Katika matokeo ya mtihani wa Taifa wa kidato cha nne mwaka 2015, jumla ya wanafunzi 568 wamefaulu mtihani na asilimia ya ufaulu kiwilaya ni 80 ikiwa ni ongezeko la ufaulu wa asilimia 0.17 ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2015.
Jedwali lifuatalo linaonyesha hali ya ufaulu wa mtihani wa kidato cha 4  kwa miaka mitatu

    Mwaka    Idadi ya watahiniwa    


Mwaka
Idadi ya watahiniwa

daraja

% ya ufaulu

I
II
III
IV
0
wav
was
wav
was
wav
was
wav
was
wav
was
wav
was
2014
333
148
6
0
41
4
78
19
131
82
57
35
79.83
2015
445
265
5
0
30
5
67
31
160
117
49
63
80
2016
409
339
3
0
44
6
77
24
209
171
76
138
71.39


Uandikishaji wa wanafunzi wa kidato cha 1 mwaka 2017
Hadi tarehe 2/02/2017  jumla ya wanafunzi 1900 sawa na asilimia 91 ya lengo la wanafunzi 2,080 walikuwa wamesharipoti shule na wanaendelea na masomo, na wanafunzi 176 sawa na asilimia 8 ya hawajaripoti katika shule walizopangiwa na majina yao yamepelekwa kwa watendaji wa kata na vijiji kwa ajili ya kubaini sababu za kutoripoti kwao ikiwa ni pamoja na kuchukuliwa hatua za kisheria kwa wazazi/walezi waliopuuza agizo la serikali la kuwapeleka shule watoto wao.
Hali ya miundombinu katika Shule za Sekondari na upatikanaji wa vitabu.
 

Miundombinu katika shule za sekondari.

NA
AINA YA MIUNDOMBINU
MAHITAJI
VILIVYOPO
PUNGUFU/ZIADA
1
Jengo la Utawala
18
14
4
2
Vyumba vya madarasa
146
135
22
3
Nyumba za walimu
266
55
211
4
Vyumba vya maabara
54
45
9
5
Viti
5842
4,594
1248
6
Meza
5842
4,803
1039
6
Vyoo ( matundu)
262
242
20

 

Halmashauri inaendelea kuboresha miundombinu ya shule, ikiwemo vyumba vya madarasa, na nyumba za walimu.

Katika kuendelea kutatua changamoto ya upungufu wa nyumba za walimu Halmashauri imepokea Tsh. 496,291,888 kutoka Serikali Kuu ambazo ni kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 2 madarasa, nyumba ya walimu (6 in 1) na vyoo matundu 8 katika shule za sekondari za Idahina na Ulewe. Fedha hizi ziko kwenye Mpango wa Maendeleo katika Elimu ya Sekondari (MMES II)

Halmashauri ya wilaya ya Ushetu inaipongeza serikali kwa kutimiza azima yake ya kutoa elimu ya msingi bila malipo yani elimu ya chekechekea hadi kidato cha nne kuanzia mwezi Disemba 2015.

Hadi kufikia sasa Halmashauri imeshapokea jumla ya Tsh. 154,110,000 kwa ajili ya elimu bila malipo ambazo zilitumwa moja kwa moja katika akaunti za shule, fedha hizi zinatumika kwa ajili ya chakula cha wanafunzi wa bweni, fidia ya ada ya bweni, fidia ya ada kwa wanafunzi wa kutwa, ununuzi wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia ambavyo ni pamoja na ununuzi wa tufe, kemikali na vivunge vya sayansi pamoja na shughuli za uendeshaji wa shule kwa ujumla.

 

Mafanikio

  • Uwepo wa maabara za sayansi katika shule zote za sekondari zilizopo katika halmashauri ya wilaya ya Ushetu.
  • Uanzishwaji wa kidato cha Tano katika shule ya sekondari ya Dakama katika tahasusi za HGL na PCM.
  •  Usimamizi bora wa ufundishaji mashuleni kunakopelekea kupanda kwa asilimia ya ufaulu kiwilaya mwaka hadi mwaka ambayo ni maendeleo ya kitaaluma.

Changamoto.

  • Upungufu wa walimu wa sayansi na hisabati, unaopelekea wanafunzi wengi kufanya vibaya zaidi katika matokeo ya mtihani wa Taifa kidato cha 4 kila mwaka. Hadi sasa upo upungufu wa walimu 75 wa sayansi na hisabati 
  •  Upungufu wa nyumba za walimu, unaotokana na ukosefu wa rasilimali fedha
  •  Baadhi ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kutoka nyumbani kuja shuleni hivyo kupelekea utoro wa mara kwa mara kwa wanafunzi hao.

Mikakati.

  • Kutumia wahitimu wa kidato cha sita kufundisha masomo ya sayansi kwa muda.
  • Kuhamasisha wananchi kujenga maboma ya nyumba za walimu na halmashauri kuendelea kutenga fedha za ukamilishaji wa maboma.
  • Kuihamasisha jamii kujenga Hosteli ili kuwajengea mazingira rafiki wanafunzi wanaoishi mbali na shule pamoja na kutatua tatizo la utoro wa wanafunzi hao.

Matangazo

  • Matokeo ya usajili wa Madereva. October 03, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • RC MACHA AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MAENDELEO YA MIRADI YA MWENGE HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU 2024/2025

    May 20, 2025
  • USHETU KUANZA KUTEKELEZA MRADI WA REA NGAZI YA VITONGOJI 151.

    May 08, 2025
  • Habari Picha: Watumishi wa Halmashauri ya Ushetu wakumbushwa kuhusu Maadili katika utumishi wa Umma

    May 07, 2025
  • Tume ya Maadili kwa watumishi wa Umma wafanya kikao na watumishi wa makao makuu Halmashauri ya Ushetu

    May 05, 2025
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0759888848

    Simu ya kiganjani: 0759888848

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa