• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA USHETU AHIMIZA USAFI,MAZOEZI UMOJA NA USHIRIKIANO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI

Ilipo tumwa: November 21st, 2025




21 oktoba,2025

Ushetu,

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, Bi. Hadij Kabojela, ametoa wito kwa watumishi wa Halmashauri kuendelea kuzingatia wajibu wao katika kutunza mazingira, kufanya mazoezi kwa ajili ya kuboresha afya zao, pamoja na kudumisha ushirikiano katika shughuli mbalimbali za kijamii na kiutendaji.


Akizungumza katika kikao maalum cha watumishi kilichofanyika katika ofisi za Halmashauri, Bi. Kabojela ameeleza kuwa utunzaji wa mazingira ni jukumu la kila mtumishi na ni msingi muhimu katika kuhakikisha jamii inapata huduma bora katika maeneo yote. Amesema kuwa mazingira safi yanachangia ustawi wa afya za wananchi na kupunguza gharama za kukabiliana na magonjwa yanayotokana na uchafu.


Katika kuhimiza afya bora kwa watumishi, Mkurugenzi amewataka kuendelea kufanya mazoezi mara kwa mara ili kuongeza tija na ufanisi kazini. Alibainisha kuwa mazoezi sio tu yanaboresha afya, bali pia yanajenga nguvu ya mwili na kuongeza uwezo wa kufikiri, hivyo kuboresha utendaji wa majukumu ya kila siku.


Aidha, Bi. Kabojela amesisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano na umoja miongoni mwa watumishi katika utekelezaji wa majukumu ya kijamii na kikazi. Amesema kuwa mshikamano na mawasiliano mazuri kati ya watumishi ni nguzo muhimu katika kufanikisha malengo ya Halmashauri na kuwatumikia wananchi kwa ufanisi.


Alihitimisha kwa kuwataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa uadilifu, uwajibikaji na kufuata maadili ya utumishi wa umma ili kuimarisha maendeleo ya Halmashauri na jamii kwa ujumla.

Matangazo

  • Matokeo ya usajili wa Madereva. October 03, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA USHETU AHIMIZA USAFI,MAZOEZI UMOJA NA USHIRIKIANO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI

    November 21, 2025
  • Halmashauri ya Ushetu Yagawa Hati za Hakimiliki za Kimila kwa Wananchi wa Vijiji vya Igunda na Butibu.

    September 27, 2025
  • HALMASHAURI YA USHETU MBIONI KUTEKELEZA MRADI WA HEWA YA KABONI.

    September 20, 2025
  • WASIMAMIZI MAGETI YA KUKUSANYA MAPATO USHETU WAPEWA MOTISHA

    September 10, 2025
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0767639345

    Simu ya kiganjani: 0767639345

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa