• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

Waziri Bashungwa akabidhi Ujenzi wa Madaraja kwa Makandarasi Ushetu

Ilipo tumwa: November 30th, 2024

WAZIRI BASHUNGWA AKABIDHI KAZI YA UJENZI WA MADARAJA KWA MAKANDARASI USHETU


Na. Emmanuel Shomary

Ushetu DC

 November 30, 2024.


WAZIRI wa Ujenzi Innocent Bashungwa amefanya ziara ya kikazi katika Halmashauri ya Ushetu Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga kukagua na kukabidhi ujenzi wa madaraja kwa makandarasi.


Ziara hiyo imefanyika leo Novemba 30, 2024, ambapo Waziri Bashungwa amesema Rais Samia ametenga kiasi cha shilingi bilioni 868 kwa ajili ya kukarabati miundombinu iliyoathiriwa na mvua za El Nino na kimbunga Hidaya kama vile barabara na madaraja.


Bashungwa amesema Halmashauri ya Ushetu imetengewa shilingi bilioni 18.5 kwa ajili ya kukarabati madaraja manne yaliyoharibiwa na mvua, likiwemo daraja linalounganisha Ushetu na Geita.


Bashungwa amefafanua kuwa Halmashauri ya Ushetu inatekeleza miradi ya ujenzi wa madaraja matatu yenye thamani ya shilingi bilioni 13.5 ambayo yatakamilika katika kipindi cha miezi 12, Pia daraja linalounganisha Ushetu na Geita lenye urefu wa mita 50 linalogharimu shilingi bilioni 5.


Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha, amemshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha za kutekeleza miradi ya ujenzi wa madaraja, akisema kuwa wananchi wa Ushetu walikuwa wakikumbwa na changamoto kubwa kutokana na hali mbaya ya miundombinu.


Mhe. Macha pia amesema kuwa Shughuli zote za maendeleo zinaunganishwa na ujenzi wa miundo mbinu ya barabara hivyo ataendelea kuwafatilia wakandarasi mpaka mirafi ikamilike, pia wananchi waitunze miradi hiyo na kuwa waaminifu kwa kulinda vifaa vyote vya ujenzi.


Aidha Macha amewaasa wananchi kulinda afya zao kwani UKIMWI upo na unauwa hivyo Miradi yote inayofanyika pasipo afya haiwezi kuwa kitu


Naye Mbunge wa Jimbo la Ushetu, Emmanuel Cherehani, ameelezea furaha ya Wananchi, akisema kuwa Serikali imejibu kiu yao ya muda mrefu ya kujengwa kwa madaraja ambayo yatakuwa na manufaa makubwa katika shughuli za kiuchumi na usafiri.


Katika hatua nyingine, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Samweli Mwambungu, ametoa taarifa kuhusu utekelezaji wa mikataba ya ujenzi wa madaraja hayo, akisema kuwa kazi zitakamilika ndani ya miezi 12 na madaraja yatakamilika kwa ubora.


Wakandarasi kutoka Kampuni ya Salum Motor Transport Limited, wanaotekeleza mradi wa daraja la Ubagwe, wameahidi kuwa mradi huo utazingatia viwango vya ubora na kukamilika kwa muda wa mkataba.


Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Ushetu bi. Martha Shija ameishukuru Serikali kwa kutatua changamoto ya madaraja kwani walikuwa wanapata shida wakati wa masika ambapo barabara zilikuwa hazipitiki kutokana na maji mengi hivyo ujenzi huo utarahisisha mawasiliano vijiji

Matangazo

  • Matokeo ya usajili wa Madereva. October 03, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • RC MACHA AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MAENDELEO YA MIRADI YA MWENGE HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU 2024/2025

    May 20, 2025
  • USHETU KUANZA KUTEKELEZA MRADI WA REA NGAZI YA VITONGOJI 151.

    May 08, 2025
  • Habari Picha: Watumishi wa Halmashauri ya Ushetu wakumbushwa kuhusu Maadili katika utumishi wa Umma

    May 07, 2025
  • Tume ya Maadili kwa watumishi wa Umma wafanya kikao na watumishi wa makao makuu Halmashauri ya Ushetu

    May 05, 2025
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0759888848

    Simu ya kiganjani: 0759888848

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa