04 Februari, 2026.
USHETU DC.
MAFUNZO hayo yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Hospitali ya Wilaya ya Halmashauri ya Ushetu, kwa muda wa siku 3, kuanzia tarehe 2-4 Feb, 2026, yalihudhuriwa na madiwani wote wa Halmashauri ya Ushetu pamoja na wakuu wa Divisheni na Vitengo, yalilenga kuwajengea uwezo kuhusu namna bora ya kuendesha na kusimamia Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Wakufunzi kutoka Taasisi ya Mafunzo ya Serikali za Mitaa, Hombolo Dodoma,
Dr. Benedict Sulley, Anorld Kabaitiraki na Bi. Nishafa Ndabakubije, wakiwasilisha mada mbalimbali kwenye mafunzo hayo, ikiwemo Uongozi na Utawala bora, ambapo walielekeza na kufundisha juu ya mambo muhimu ya kuzingatia ili kutimiza adhima ya Utawala na uongozi bora kwenye taasisi.
Katika hatua nyingie, Mada za Sheria za Uendeshaji wa Shughuli za Serikali za Mitaa, Muundo, Majukumu na madaraka ya serikali za mitaa na Uendeshaji wa Vikao na matukio katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, ziliwashirishwa kwa ufasaha na wajumbe walipata muda wa kuuliza maswali na kufanya mijadala.
Kwa upande wa mwingine, Mada zinazohusu Mipango, Bajeti na Usimamizi wa miradi ya maendeleo, Usimamizi na udhibiti wa fedha katika Mamlaka za Serikali za Mitaa pamoja na Usimamizi wa Watumishi na Usimamizi wa Ardhi katika mamlaka ya Serikali za Mitaa, pia ziliwasilishwa.
Mawasilisho mengine yalihusu Wajibu, Majukumu, Haki na Stahiki za Diwani na pia Maadili ya Madiwani, zilifundishwa katka mafunzo hayo.
Wakizungumza wakati wa kuhitimisha mafunzo hayo, Madiwani wa Halmashauri ya ushetu, Wameipongeza Serikali ya mama Samia, kwa kuendelea kuleta fedha nyingi za miradi ya maendeleo kwenye Halmashauri ya Ushetu, na kwa mafunzo waliyoyapata, wameahidi kuongeza ufanisi katika kusimamia na kutekeleza miradi yote ya maendeleo kwenye kata zao.
Na kwa upande mwingine, Madiwani hao, wamemshukru na kumpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu, Bi. Hadija Kabojela kwa kuwaandalia mafunzo hayo muhimu.
Halmashauri ya Ushetu, inajumla ya Madiwani 27, 20 wakiwa wa kuchaguliwa na 7 ni madiwani wa viti maalumu, huku ikiwa na jumla ya kata 20, vijiji 112 na jumla ya vitongoji 554.
Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Anuani: S. L. P 50 Kahama
Simu: 0767639345
Simu ya kiganjani: 0767639345
Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz
Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa