• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

U.S. CDC NA THPS WAKABIDHI KLINIKI YA TIBA NA MATUNZO YA VVU ILIYOKARABATIWA YA BULUNGWA NA VIFAA MBALIMBALI KWA HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU.

Ilipo tumwa: March 15th, 2024


 

Na. Ushetu Dc, KAHAMA.

SHIRIKA la Tanzania Health Promotion Support (THPS), leo 15 machi, 2024, limekamilisha ukarabati wa Kituo cha tiba na matunzo ya Virusi vya UKIMWI (VVU) ya Kituo cha Afya  Bulungwa kilichopo Kata ya Bulungwa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, Mkoani Shinyanga na kukabidhi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu.

Zoezi la ukarabati liligharimu jumla ya TZS. 204,468,950 (USD M81,787.58) ikiwa ni sehemu ya mradi wa Afya Hatua, unaofadhiliwa na Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na UKIMWI (PEPFAR) kupitia Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa cha Marekani (U.S.CDC)

Kituo kiliimarishwa ili kuhakikisha Wananchi wengi zaidi katika Halmashauri ya Ushetu wanapata huduma bora za afya na matibabu na hii ni pamoja na kubomoa jengo, uashi, vyuma, kuezeka paa, mfumo wa kutupa maji ya mvua, milango na madirisha, finishes, samani, usafi wa mitambo, usambazaji wa maji. mabomba, mifereji ya maji taka na mfumo wa uingizaji hewa, vifaa vya mabomba na mfumo wa umeme.

Dk. Daniel Magesa, Mkuu wa Tawi la Huduma za Kliniki kutoka U.S.CDC Tanzania ameungana na Bw. George Anatory, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa THPS, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa THPS katika kukabidhi rasmi kituo hicho kilichofanyiwa ukarabati kwa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu Bi. Hadija Mohamed KABOJELA ambaye ni mgeni rasmi akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita katika hafla hiyo iliyofanyika katika viwanja vya kituo cha Afya Bulungwa. Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mganga Mkuu wa Halmashauri  ya Ushetu, watumishi wa Kituo cha Afya Bulungwa na watumishi wa THPS wakishuhudia tukio hilo.

Akizungumza katika hafla hiyo Bi. Kabojela alitoa shukurani zake kwa msaada mkubwa unaotolewa na Serikali ya Marekani kupitia THPS katika kudhibiti janga la UKIMWI na kuokoa maisha ya wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu. Aliahidi kudumisha ushirikiano unaohitajika na CDC na THPS ili kuendeleza mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI.

Kwa upande wake Dk. Magesa alieleza kuwa serikali ya Marekani inaitambua na kuipongeza Wizara ya Afya, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa (TAMISEMI), viongozi wa mikoa, mamlaka za serikali za mitaa, mashirika yasiyo ya kiserikali na asasi za kiraia kwa dhamira ya kuboresha matokeo ya afya nchini Tanzania. Alisisitiza kuwa kuongezeka kwa ushirikiano  katika kinga, tiba na matunzo ya VVU na UKIMWI kutasaidia kuimarisha utoaji wa huduma bora za afya na VVU, huku akisema Serikali ya Marekani inatambua na kuunga mkono ahadi hii.

Katika hatua nyingine, Kituo hicho kipya kilichokarabatiwa,  kinatarajiwa kuweka mazingira bora ya kutoa huduma za tiba na matunzo  ya VVU na hivyo kusababisha ongezeko la watu wanaopata huduma katika kituo hicho.

Katika maelezo yake Bw.George Anatory, alisema shirika lake limejipanga kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuhakikisha watanzania wote wanapata huduma bora za afya na kuchangia kikamilifu katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi Nchini.

Bw.Anatory, alisisitiza umuhimu wa matumizi sahihi na matengenezo ya kituo hicho ili kuhakikisha utoaji wa huduma bora za tiba na matunzo ya VVU sambamba na kuhimiza ufuasi wa huduma za tiba ya ARV kwa wapokea huduma.

"Nina imani kuwa msaada tuliotoa utaboresha utoaji wa huduma za kinga, tiba na matunzo ya VVU, na kusaidia kuokoa maisha katika wilaya ya Ushetu na maeneo jirani", alisema.

 

Kuhusu THPS

Tanzania Health Promotion Support (THPS) ni asasi isiyo ya kiserikali iliyoanzishwa mwaka 2011, chini ya Sheria ya asasi zisizo za kiserikali nambari 24 ya 2002.

THPS inafanya kazi kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara za Afya za Tanzania Bara na Zanzibar; Wizara ya Jinsia, Vijana, Wazee na Makundi Maalum; Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Kwa ufadhili wa Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Misaada ya UKIMWI kupitia Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa, THPS  inatekeleza afua mbalimbali za VVU/UKIMWI; Kifua kikuu; kuzuia ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto; huduma za afya ya uzazi, uzazi, watoto wachanga, watoto na vijana; mifumo ya habari ya maabara na usimamizi wa afya, na UVIKO-19.

Kuhusu mradi wa CDC/PEPFAR Afya Hatua (Oktoba, 2021- Septemba, 2026)

Mradi huu unalenga kutoa huduma jumuishi katika vituo vya afya (Kigoma, Pwani, Shinyanga na Tanga) na katika jamii (Kigoma, Pwani na Tanga). Huduma hizi ni pamoja na matibabu na matunzo ya watu wanaoishi na VVU, huduma za kitabibu za tohara kwa wanaume katika mikoa ya Kigoma na Shinyanga na programu ya DREAMS kwa wasichana balehe na wanawake wadogo katika mkoa wa Shinyanga.

Matangazo

  • Matokeo ya usajili wa Madereva. October 03, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • RC MACHA AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MAENDELEO YA MIRADI YA MWENGE HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU 2024/2025

    May 20, 2025
  • USHETU KUANZA KUTEKELEZA MRADI WA REA NGAZI YA VITONGOJI 151.

    May 08, 2025
  • Habari Picha: Watumishi wa Halmashauri ya Ushetu wakumbushwa kuhusu Maadili katika utumishi wa Umma

    May 07, 2025
  • Tume ya Maadili kwa watumishi wa Umma wafanya kikao na watumishi wa makao makuu Halmashauri ya Ushetu

    May 05, 2025
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0759888848

    Simu ya kiganjani: 0759888848

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa