• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

Mvua Kubwa yaleta Uharibifu Mkubwa Kijiji cha Butibu Kata ya Kinamapula - Ushetu

Ilipo tumwa: November 15th, 2022

MVUA KUBWA YALETA UHALIBIFU MKUBWA WA NYUMBA NA MAKAZI YA WATU KATIKA KIJIJI CHA BUTIBU KATA YA KINAMAPULA WILAYANI KAHAMA.

Butibu-Kinamapula, Ushetu.

Mvua zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali Nchini, zimesababisha uhalibifu  mkubwa wa nyumba na makazi ya watu katika kijiji cha Butibu kata ya Kinamapula wilayani Kahama.

Mvua hizo zilizoamabatana na upepo mkali, ngurumo na radi, zilianza kunyesha majira ya saa 10 alfajiri usiku wa kuamkia Jumanne Novemba 15, 2022, katika kijiji hicho, zilisababisha uhalibifu mkubwa ambapo jumla ya Majengo matatu  (3) ya Taasisi na Majengo kumi na nne (14) ya watu binafsi yameharibika.

Majengo matatu ya Taasisi za Umma yaliyoharibiwa ni pamoja na:

  1. Madarasa manne, Ofisi mbili na Nyumba moja ya Mwalimu Shule ya Msingi Butibu, Butibu A
  2. Kanisa la Roman Cathoric (RC) na Sabato, Butibu B.
  3. Godauni la Chama cha Msingi, Butibu A.




Picha 1: Jengo la kanisa Katoriki Butibu lililoezuliwa paa.

Katika hatua nyingine, nyumba  kumi na nne (14) za makazi ya watu binafsi zilizoharibiwa ni kama ifuatavyo:

Na.
Jina la mwenye Nyumba
Kitongoji
Madhara kwenye Nyumba
1
Hayati, Elias John  Kwandikwa
Butibu A
Ukuta wa Fensi Umeanguka
2
Phabiani Stephano
Butibu A
Paa Limeezuliwa
3
Suzana Willium
Butibu A
Paa Limeezuliwa
4
Daudi Kanindo
Butibu A
Paa Limeezuliwa
5
Annastazia Martine
Butibu A
Paa Limeezuliwa
6
Joel Ernest
Butibu A
Paa Limeezuliwa
7
Mihangwa Lusupya
Shinyanga
Paa Limeezuliwa
8
Mateso Ramadhani
Shinyanga
Paa Limeezuliwa
9
Veronica Samsoni
Butibu B
Paa Limeezuliwa
10
Julius Kitobelo
Butibu B
Paa Limeezuliwa
11
Kulwa Kasala
Butibu B
Paa Limeezuliwa
12
Nyorobi Gamuga
Butibu B
Imeanguka
13
Charles Maziku
Nkuruungu A
Paa Limeezuliwa
14
Enos Majebele
Nkurungu A
Paa Limeezuliwa

Pamoja na uhalibifu huo, Mvua hizo pia zimesababisha wakazi watatu wa kijiji cha Butibu kudhulika ambapo bwana Julius Kitobeho aliangukiwa na tofali sehemu za kiunoni wakati akiwa katika harakati za kujiokoa na mvua hizo, ambapo hali yake inaendelea vyema bada ya kupatiwa matibabu katika zahanati ya Butibu kijijini hapo.

Kwa Upande mwingine, bwana na Bi Juma Ngulya nao walipata madhara ya kujeruhiwa na nyumba yao iliyobomolewa na mvua hizo, ambapo walipelekwa katika Hospitali ya Wilaya Kahama na hali zao zinaendelea vyema.



 

Picha 2: Jengo la darasa katika shule ya Msingi Butibu Lililobomolewa na Mvua hizo.

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Butibu, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ushetu, Ndugu Linno P. Mwageni, amewapa pole Wananchi hao na pia kuwapa elimu ya namna ya kujikinga na madhara ya mvua, na katika hatua nyingine amewataka Wananchi hao kuwa watulivu katika kipindi hiki, ambapo Serikali inaandaa utaratibu wakuwasaidia Wananchi hao waliodhurika na Mvua hizo.

Picha 3: Nyumba ya ndg Julius Kitobelo iliyobomolewa na Mvua hizo.

 




 

Picha 4: Ukuta wa fensi ya nyumba ya hayati Elias Kwandikwa ulioanguka.



 

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA USHETU YAGAWA PIKIPIKI 44, KWA MAAFISA UGANI 38 NA WATENDAJIWA KATA 6.

    March 02, 2023
  • “HAKUNA MABADILIKO YOYOTE YATAKAYOFANYIKA KATIKA NCHI HII BILA NINYI WAALIMU KUSHIRIKI KIKAMILIFU”- MWAGENI, DED USHETU DC.

    January 09, 2023
  • Habari Picha: Matukio ya kijamii katika maadhimisho ya siku ya Mama na Mtoto

    December 07, 2022
  • Taarifa kwa Umma

    November 18, 2022
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0759888848

    Simu ya kiganjani: 0759888848

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa