• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

“MRADI HUU WA STADI ZA MAISHA KWA WANAFUNZI, KWETU UMEKUJA KWA WAKATI SAHIHI SANA” - Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Ushetu.

Ilipo tumwa: June 11th, 2024

“MRADI HUU WA STADI ZA MAISHA KWA WANAFUNZI, KWETU UMEKUJA KWA WAKATI SAHIHI SANA” - Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Ushetu.


Na Emmanuel Shomary

Ushetu DC

11 Juni, 2024.



Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ushetu Bi. Hadija KABOJELA, amewashukuru sana Serikali ya Tanzania kwa Kusirikiana na Mdau CAMFED kwa kuleta Mradi wa  Stadi za Maisha kwa Wanafunzi wa Sekondari katika Halmashauri ya Ushetu.


Hayo ameyasema leo  11 Juni, 2024  wakati akifungua  mafunzo ya siku 2  yanayofanyika katika ukumbi  wa Hospitali ya Wilaya ya Ushetu  na kuhudhuriwa na Maafisa Elimu Kata, Wakuu wa Shule,  Walimu Walezi pamoja na maafisa elimu ngazi ya Halmashauri.


“Kwetu sisi Mradi huu umekuja wakati sahihi sana, Ombi langu  kwa washiriki wote, Maafisa Elimu Kata, Wakuu wa Shule na Walimu Walezi hakikisheni mradi huu unafanikiwa ili watoto wetu wapate ujuzi utakaowasaidia katika Maisha yao ya baadae.

Naamini kwa kushirikiana na CAMFED Tanzania, tunaweza kuchochea maendeleo ya jamii yetu” alisema bi.  Kabojela.


Katika hatua nyingine,  Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Ushetu, ndugu Emmanuel Clement MALIMA, amewasisitizia walimu hao kuyafanyia kazi mafunzo hayo yanayotolewa na CAMFED ili kuweza kuondoa tatizo la watoto wanaoacha shule kwa sababu mbalimbali.


“Niwaombe walimu, sisi ndio wadau wenye mradi huu, tuhakikishe tunashirikiana pamoja ili tumkomboe mtoto wa Ushetu katika suala la kushindwa kumaliza masomo yake” alisema Malima.


Awali akitambulisha mradi huo, Kiongozi wa mradi wa Stadi za Maisha kutoka CAMFED  Bwana  James Mussa Mnyeti, amewaomba washiriki wa mafunzo hayo kuupokea mradi huo kwa mikono miwili kwani umekuwa na mafanikio makubwa katika kuboresha maendeleo ya wanafunzi.


Mradi wa CAMFED unafanya kazi katika Nchi tano barani Afrika Ghana, Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe. Na kwa Tanzania ulianza mwaka 2006 na unafanya kazi katika Mikoa kumi, Shinyanga, Morogoro, Pwani, Tanga, Tabora, Singida, Dodoma, Mwanza, Iringa na Dar es salaamu.

Kwa mkoa wa Shinyanga CAMFED, Inafanya kazi kwenye Halmashauri nne, Ushetu, Kishapu, Msalala na Shinyanga DC.

Matangazo

  • Matokeo ya usajili wa Madereva. October 03, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • USHETU KUANZA KUTEKELEZA MRADI WA REA NGAZI YA VITONGOJI 151.

    May 08, 2025
  • Habari Picha: Watumishi wa Halmashauri ya Ushetu wakumbushwa kuhusu Maadili katika utumishi wa Umma

    May 07, 2025
  • Tume ya Maadili kwa watumishi wa Umma wafanya kikao na watumishi wa makao makuu Halmashauri ya Ushetu

    May 05, 2025
  • Tangazo la uuzaji Viwanja vya Makazi na Viwanda vidogo.

    April 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0759888848

    Simu ya kiganjani: 0759888848

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa