• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA USHETU.

Ilipo tumwa: July 27th, 2025

Na. Emmanuel Shomary,

Ushetu DC

Jumamosi, 26 Julai, 2025.


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, ameendelea na ziara yake ya kikazi katika wilaya za Mkoa huo kwa lengo la kujionea hatua ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ambapo leo Julai 26, 2025, ametembelea Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu na kupongeza juhudi kubwa zinazofanywa katika kusimamia Miradi inayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja.


Katika ziara hiyo, Mhe. Mhita ametembelea miradi kadhaa ikiwemo Ujenzi wa Shule ya Msingi Igwamanoni kata ya Igwamanoni inayolenga kupunguza msongamano wa wanafunzi na kuongeza upatikanaji wa elimu bora kwa watoto.

 Aidha, alikagua ujenzi wa mashine ya kuchakata mazao ya kilimo uliopo kata ya Bulungwa, ikiwa ni hatua ya kuwawezesha wakulima kuongeza thamani ya mazao yao na kukuza uchumi wa kaya.


Vilevile, Mkuu huyo wa Mkoa alitembelea Kituo cha Afya Bulugwa ambako ujenzi wa wodi ya wazazi unaendelea. Mradi huo unatarajiwa kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto kwa kupunguza umbali wa kufuata huduma hizo.


 Miradi mingine ni pamoja na upandaji miti uliopo shule ya msingi Butibu, kata ya Kinamapula, kwa ajili ya uhifadhi wa mazingira.


Pia alikagua ujenzi wa tanki kubwa la maji na mtandao wa usambazaji maji safi na salama katika maeneo ya vijijini, uliopo kata ya Bukomela pamoja na ujenzi wa shule mpya ya Amali iliyopo kata ya Nyamilangano ambayo itasaidia kuwapa vijana elimu ya ufundi na kuwajengea uwezo wa kujiajiri.


Akizungumza baada ya kutembelea miradi hiyo, Mhe. Mhita amesema ameridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo, usimamizi wake na jinsi inavyolenga kuboresha maisha ya wananchi. Amewapongeza viongozi na watendaji wa halmashauri ya Ushetu kwa kushirikiana na wananchi kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa viwango na ndani ya muda.


Aidha, Mhe. Mhita amehimiza usimamizi madhubuti wa miradi yote ya serikali ili kuhakikisha rasilimali zinazotolewa zinatumika kwa uaminifu na kuleta tija kwa wananchi. Ameongeza kuwa ni muhimu kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika kutunza miundombinu hiyo ili idumu na kuendelea kutoa huduma kwa vizazi vijavyo.


 “Mkoa wa Shinyanga una fursa kubwa ya maendeleo, ni wajibu wetu wote kuhakikisha tunazitumia kikamilifu. Halmashauri ya Ushetu imeonyesha mfano mzuri kwa usimamizi wa miradi, tunataka kuona kila halmashauri inakwenda kwa kasi hii,” amesema Mhe. Mhita.


Ziara ya mkuu huyo wa mkoa ni sehemu ya utaratibu wa kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhimiza uwajibikaji kwa watendaji wa serikali ili kufanikisha ajenda ya maendeleo ya Taifa.

Matangazo

  • Matokeo ya usajili wa Madereva. October 03, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • "Swala la Lishe sio la hiari, Utekelezaji wake ni wa lazima"- DC Frank Nkinda.

    July 30, 2025
  • MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA USHETU.

    July 27, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU YASHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA ZA AFYA.

    July 24, 2025
  • Bodi ya Afya ya Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu yazinduliwa.

    July 11, 2025
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0759888848

    Simu ya kiganjani: 0759888848

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa