• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

MHE. MTATIRO AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU.

Ilipo tumwa: June 28th, 2024

MHE. MTATIRO AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU.

Na. Emmanuel Shomary, USHETU DC.

MUWAKILISHI wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Julius Mtatiro (Adv) ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu kwa kuonesha uwezo mkubwa wa kuandaa, kujibu, na kuwasilisha hoja zinazohusu Utekelezaji wa Mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo ilikuwa na jumla ya hoja 32 na 16 kati ha hizi zilikaguliwa na kufungwa, 15 zipo kwenye hatua ya utekelezaji huku 1 haijatekelezwa huku akimtaja Bi. Hadija Kabojela kama Mkurugenzi na mwanamama wa kuigwa kama mfano.

Mhe. Mtatiro ameyasema leo tarehe 27 Juni, 2024 katika Baraza Maalum la CAG ambapo pamoja na mambo mengine Mhe. Mtatiro amewapongeza sana Waheshimiwa Madiwani wote na kipekee kwa Waheshimiwa wanamama ambao wameonesha uwezo mkubwa sana wa kuchambua, kujenga na kupambania hoja kwa lengo la kuiletea maendeleo Ushetu, kutetea haki na mali za Wanaushetu tena kwa kutumia na kusoma Kabrasha kwa kujiamini, utulivu na uzalendo mkubwa zaidi.

"Kwa dhati kabisa naipongeza sana Ushetu DC kwa namna ambavyo mmeonesha uwezo mkubwa wa kuandaa, kujibu na kuwasilisha taarifa zenu zinazohusu mapendekezo ya CAG, pia waheshimiwa madiwani wote hasa wanamama, mwenyekiti wa Halmashauri Mhe.Gagi Lala, Mkurugenzi wa Ushetu Bi. Hadija Kabojela na watalaam hakika mnastahili pongezi hizi mmekuwa mfano wa kuigwa kulinganisha na Halmashauri nyingine ambazo nimepita na kuona utekelezaji wa hili," amesema Mhe. Mtatiro.

Ushetu inatajwa kuwa na hoja chache zaidi kulinganisha na Halmashauri nyingine hapai Shinyanga ambapo hoja za nyuma zilikuwa 78, zimejibiwa 70 na kubakia 8 ambazo zipo kwenye hatua ya utekelezaji jambo ambalo limepongezwa sana pia na Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumbo ambaye amesema kuwa kipekee ameshuhudia mshikamamo mkubwa wa madiwani, Mhe. Mbunge na wataalam wakiongozwa na Mkurugenzi Bi. Hadija Kabojela.

Akiahirisha mkutano huu, Mhe. Gagi amesema kuwa anapokea pongezi hizi zote, maelekezo na ushauri uliotolewa wote na kwamba wanakwenda kuanza kutekeleza huku akisisitiza kuwa kwa kauli moja, baraza la madiwani linaazimia na kuelekeza kuwa wale wote wanaodaiwa kutokana na mkopo wa fedha za asilimia 10 za wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ambao hawajalipa watafutwe na walipe fedha hizo ili Halmashauri iweze kuondokana na hoja za CAG na pia kwa kufanya hivyo kutawezesha na wengine kukopa na hivyo kuinua uchumi wa wananchi wa Ushetu.

Matangazo

  • Matokeo ya usajili wa Madereva. October 03, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • RC MACHA AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MAENDELEO YA MIRADI YA MWENGE HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU 2024/2025

    May 20, 2025
  • USHETU KUANZA KUTEKELEZA MRADI WA REA NGAZI YA VITONGOJI 151.

    May 08, 2025
  • Habari Picha: Watumishi wa Halmashauri ya Ushetu wakumbushwa kuhusu Maadili katika utumishi wa Umma

    May 07, 2025
  • Tume ya Maadili kwa watumishi wa Umma wafanya kikao na watumishi wa makao makuu Halmashauri ya Ushetu

    May 05, 2025
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0759888848

    Simu ya kiganjani: 0759888848

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa