• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

JUMLA YA MIFUGO WAPATAO 298,024 KUPATIWA CHANJO YA HOMA YA MAPAFU, USHETU.

Ilipo tumwa: September 2nd, 2025



Na. Emmanuel Shomary

Ushetu DC.

01 Septemba, 2025.


Jumla ya mifugo wapatao  298,024 wakiwemo Ng’ombe,Kondoo na Mbuzi wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya homa ya mapafu katika halmashauri ya Ushetu wilani Kahama mkoani Shiyanga.


Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, bwana Deus Kakulima wakati akizindua chanjo hiyo katika kijiji cha Chambo  kata ya Chambo Halmashauri ya Ushetu.


Kakulima amesema kuwa Zoezi la chanjo ya homa ya mapafu kwa mifugo Halmashauri ya Ushetu  limeanza tarehe 1 Septemba na litatamatika tarehe 20 Septemba mwaka huu na linatarajiwa kufika katika kata zote 20 za halmashauri hiyo.


“Zoezi hili tumelianza leo Septemba 1 na tunatarajia kufika katika kata zote 20 vijiji 112 na tutahitimisha Septemba 20 mwaka huu ambapo jumla ya mifugo 298,024 wakiwemo Kondoo mbuzi na Ngombe wanatarajia kuchanjwa chanjo ya homa ya Mapafu” Amesema Kakulima.


Sambamba na hayo Kakulima ametoa wito kwa wafugaji wote kupeleka mifugo yao kupatiwa chanjo hiyo muhimu ambayo inatolewa kwa kwa ruzuku ya serikali na mfugaji atachangia kiasi kidogo kwa kila mfugo.


“Nitoe rai kwa wafugaji wote leteni mifugo yenu katika  maeneo ya kuchanjia ili kufanikisha chanjo hii muhimu kwa mifugo yetu ambayo huduma hii tunaitoa kwa fedha za ruzuku ya serikali na mfugaji atatakiwa kuchangia shilingi 500 kwa kila ng’ombe na shilingi 300 kwa ng’ombe na kondoo” Ameongezea Kakulima.


Akiongea kwa niaba ya wafugaji wenzake bwana Donald Mtogwa kutoka kijiji cha Chambo wameishukru Serikali ya awamu ya sita kwa kuwaletea huduma hiyo muhimu kwani awali walikuwa wanatumia fedha nyingi kununua chanjo mitaani.


“Sisi wafugaji, tunasema Asante sana kwa Serikali yetu kwa kutuletea huduma hii muhimu, kwani mara kadhaa tumekuwa tukipatwa na kadhia hii ya kupoteza mifugo yetu,lakini wakati mwingine tumekuwa tukinunua chanjo hizo kwa bei kubwa mitaani lakini sasa mifugo yetu itastawi sana na itakuwa salama” Amesema Bwana Mtogwa.


Zoezi hilo linalenga kupunguza vifo vya mifugo kwa wafugaji kwenye Halmashauri hiyo,kutokana na matukio mengi ya wafugaji kupoteza mifugo yao kutokana na ugonjwa wa homa ya mapafu,Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu  ina jumla ya Ng'omb 190,000,Mbuzi 84,688 na Kondoo 24,336.

Matangazo

  • Matokeo ya usajili wa Madereva. October 03, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • JUMLA YA MIFUGO WAPATAO 298,024 KUPATIWA CHANJO YA HOMA YA MAPAFU, USHETU.

    September 02, 2025
  • TAKUKURU – KAHAMA: USHIRIKISHWAJI WA MAKUNDI MBALIMBALI

    August 21, 2025
  • TAKUKURU Wilaya ya Kahama watoa elimu ya Mafunzo juu ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa kwa watumishi wa Afya wa Hospitali ya Wilaya ya Ushetu.

    August 12, 2025
  • TAKUKURU Wilayani Kahama yawafunda watumishi wa Idara ya Afya Kituo cha Afya Bulungwa.

    August 15, 2025
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0767639345

    Simu ya kiganjani: 0767639345

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa