• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU YASHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA ZA AFYA.

Ilipo tumwa: July 24th, 2025

Na. Emmanuel Shomary,

Ushetu DC

Alhamis, 24 Julai, 2025.


Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu,  Wilayani Kahama, Mkoani  Shinyanga, imeshika nafasi ya tatu (3) Kitaifa katika viashiria vya utoaji wa huduma bora za afya.


Haya yamesemwa leo tarehe 24 Julai, 2025 na Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo

Dkt.  Athuman Yusuph Matindo, wakati wa Kikao kazi kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Hospitali ya Wilaya ya Ushetu na  kuhudhuriwa na Mgeni rasmi ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ushetu, Bi. Hadija Kabojela, CHMT yote ya Ushetu, pamoja Waganga wafawidhi wote kutoka Zahanati,  Vituo vya Afya na Hospitali ya Halmashauri ya Ushetu.


Akisoma taarifa ya Utoaji wa Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kwa Mgeni rasmi, Dkt. Matindo alisema, Divisheni imefanikiwa kwa kiwango kikubwa katika kuboresha Huduma za Afya, ikiwa ni pamoja na Upatikanaji wa Dawa Muhimu, Vifaa tiba na Vitendanishi kwa kiwango cha 95.6% kutoka 86.2% ya mwaka 2023/2024.


Katika hatua nyingine, Dkt. Matindo ameeleza kuwa, Divisheni imefanikiwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa Mapato kutoka Tsh. 400 milioni, iliyokuwa bajeti ya mwaka 2024/2025 na kukusanya kiasi cha Tsh. 1.04 bilioni, ikiwa ni ongezeko la 210% ya lengo lake la ukusanyaji wa Makusanyo ya Uchangiaji wa huduma kwa mwaka husika.


"Ndugu  Mkurugenzi, Divisheni imefanikiwa kwa kiwango kikubwa katika ukusanyaji wa makusanyo ya kuchangia huduma za Afya, hali hiyo pamoja na mengine mengi, yamepelekea Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu kushika nafasi ya tatu Kitaifa katika Viashiria vya Utoaji Huduma bora", alieleza Dkt. Matindo.


Katika hatua nyingine,  Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Ushetu,  Bi. Kabojela, amepongeza sana juhudi hizo na kuahidi kuendelea kushirikiana vema na Divisheni hiyo ili kuboresha zaidi Huduma za Afya Ushetu.


" Nimefurahi sana kwa mafanikio haya makubwa mmepata kama Divisheni na Halmashauri kwa ujumla, mm ninaahidi kuendelea kushirikana na ninyi kwa ukaribu zaidi kwa kila hatua, ili kuleta ufanisi wa utoaji bora wa huduma za Afya ndani ya Halmashauri yetu", alisema Bi. Kabojela.


Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, inajumla  ya Zahanati 32, Vituo vya Afya 5 na Hospitali 1, huku ikiwa na jumla ya  watumishi 365 wa ajira za kudumu na watumishi 84 wa ajira za Mkataba, idaidi hii ya watumishi waliopo ni sawa na 70% ya mahitaji halisi.


Matangazo

  • Matokeo ya usajili wa Madereva. October 03, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • "Swala la Lishe sio la hiari, Utekelezaji wake ni wa lazima"- DC Frank Nkinda.

    July 30, 2025
  • MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA USHETU.

    July 27, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU YASHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA ZA AFYA.

    July 24, 2025
  • Bodi ya Afya ya Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu yazinduliwa.

    July 11, 2025
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0759888848

    Simu ya kiganjani: 0759888848

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa