Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu kupitai ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019 inaendelea na zoezi la uandikishaji wa orodha ya wapiga kura watakaoshiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 24/11/2019.
Uandikishaji orodha ya wapiga kura ambao umeanza tarehe 8/10/2019 unafanyika kwa mujibu wa kanuni na mwongozo wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2019. Kwa siku ya saba tarehe 14 Oktoba 2019 jumla ya wapiga kura 16,289 wakiwemo wanaume 7,002 na wanawake 9,289 wamejiandikisha. Aidha jumla ya wapia kurawa 90,850 (wakiwemo 43,625 wanaume na 47,280 wanawake) wamejiandikisha tangu siku ya kwanza mpaka sasa sawa na 61% ya wapiga kura 148,244 waliotarajiwa kwa mujibu ya malengo yaliyotolewa na OR – TAMISEMI.
Uandikishaji huo uliopangwa kufanyika kuanzia tarehe 8 – 14 Oktoba 2019 sasa unaendelea hadi tarehe 17 Oktoba 2019 baada ya Waziri wa Nchi OR – TAMISEMI kufanya marekebisho ya ratiba ya uandikishaji wa orodha ya wapiga kura tarehe 13 Oktoba kwa kuongeza muda wa siku tatu za ziada katika zoezi hilo.
Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Anuani: S. L. P 50 Kahama
Simu: 0759888848
Simu ya kiganjani: 0759888848
Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz
Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa