• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA USHETU, AKUTANA NA WADAU KUJADILI NAMNA BORA YA KUBORESHA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

Ilipo tumwa: August 8th, 2024


Na. Emmanuel Shomary,

Ushetu DC.

Katika kuelekea zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la  wapiga kura,  Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama Mkoani Shinyanga, imekutana na wadau mbalimbali  ili kujadili namna bora ya uhamasishaji  Wananchi kujitokeza kwa wingi  katika zoezi hilo linalotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Kikao hicho kimefanyika Agosti  7, 2024  katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu, huku zoezi hilo likitarajia kushika hatamu kuanzia Agosti 21 mpaka  27 mwaka, huku kukiwa na Vituo 249 vya uandikishaji  katika Halmashauri hiyo.

Akiongea katika kikao hicho, Afisa mwandikishaji wa Jimbo la Ushetu, Bi. Hadija  Kabojela,  amewaomba wadau wote waliojitokeza kuwa mabalozi Wazuri katika kuihamasisha jamii kuona umuhimu wa kushiriki  zoezi hilo la  kuboresha taarifa zao , sambamba na kujiandikisha upya kwa wale wenye sifa.


Bi. Kabojela amesema wadau ni chachu ya maendeleo hivyo Wana wajibu wa kushiriki zoezi  la  uhamasishaji wa Uboreshaji wa Daftari  la Kudumu la wapiga kura  kwa kutoa taarifa na elimu sahihi juu ya  umuhimu  huo wa kujiandikisha kwani kwa kufanya hivyo kutamsaidia raia kutimiza haki yake ya msingi katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2025 kwa kupiga kura kwa Kiongozi anaye mtaka.


Kwa Upande wake Afisa Uchaguzi wa Jimbo la Ushetu Bw. Elisha MAHUNGO, ametaja wenye sifa za kushiriki katika zoezi hilo la Uboreshaji wa Daftari Kudumu la wapiga kura ni pamoja na Wapiga Kura wapya ambao hawajawahi kujiandikisha lakini Wana sifa za kupiga kura kuanzia miaka 18 na kuendelea,  wale wote watakaotimiza miaka 18 ifikapo Oktoba kipindi Cha uchaguzi Mkuu mwaka 2025, lakini pia wale waliohamia kwa makazi ya kuishi katika Jimbo hilo, waliopoteza kadi zao, sambamba na kufuta taarifa za wapiga kura waliokosa sifa za kuendelea kuwepo katika Daftari hilo hasa waliotangulia mbele za haki.


Sambamba na hilo, alisema zoezi hilo halitawahusu Wananchi walio na vitambulisho  visivyohitaji maboresho, hivyo amewasihi kuendelea kuvitunza kwa umakini mkubwa.


Kikao hicho kimehudhuliwa na wadau mbalimbali likiwemo Shirika la Huheso, Jeshi la Polisi Ushetu, Viongozi wa dini, viongozi wa vyamba vya Siasa, wawakilishi wa vijana, pamoja na Vikundi vya hamasa vinavyopatikana ndani ya Halmashauri ya Ushetu.

Matangazo

  • Matokeo ya usajili wa Madereva. October 03, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • USHETU KUANZA KUTEKELEZA MRADI WA REA NGAZI YA VITONGOJI 151.

    May 08, 2025
  • Habari Picha: Watumishi wa Halmashauri ya Ushetu wakumbushwa kuhusu Maadili katika utumishi wa Umma

    May 07, 2025
  • Tume ya Maadili kwa watumishi wa Umma wafanya kikao na watumishi wa makao makuu Halmashauri ya Ushetu

    May 05, 2025
  • Tangazo la uuzaji Viwanja vya Makazi na Viwanda vidogo.

    April 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0759888848

    Simu ya kiganjani: 0759888848

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa