• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

"Swala la Lishe sio la hiari, Utekelezaji wake ni wa lazima"- DC Frank Nkinda.

Ilipo tumwa: July 30th, 2025


Na. Emmanuel Shomary,

Ushetu DC

Jumanne, 29 Julai, 2025.


MKUU wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Frank Nkinda, amesema hayo leo terehe 29 Julai, 2025 kwenye kikao cha tathimini ya lishe, kilichofanyika kwenye ukumbi wa vikao uliopo  Hospitali ya wilaya ya Ushetu na kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali akiwemo Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi. Hadija Kabojela.


Akiongea katika kikao hicho, Mhe. Nkinda amewataka watendaji wa kata na wote wanaotekeleza afua za lishe, kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuweza kufikia malengo kusudiwa.

"Swala la lishe sio la hiari, maana utekelezaji wake ni wa lazima, kwani haya ni maagizo ya Mhe. Rais, hivyo niwaombe mshirikiane na wanasiasa na wadau wengine, ili mnapokuwa huko vijijini kuwapa elimu Wananchi, inakuwa rahisi kama mkiwashirikisha wanasiasa na wadau wengine walio na ushawishi kwa jamii hiyo" amesema mhe. Nkinda.


Katika hatua nyingine, Mhe. Mkuu wa Wilaya, amewapongeza watendaji wa vijiji na Kata, kwa kazi nzuri wanazofanya katika kutekeleza afua za lishe na kuwataka waendelee kushirikishana uzoefu ili kwa pamoja wafikie malengo kusudiwa kwenye swala zima la lishe.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu, amewapongeza Divisheni ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii pamoja na watendaji wa kata, kwa juhudi wanazofanya katika kutekeleza afua za lishe.

"Halmashauri imeendelea kufanya vema kwenye utekelezaji wa afua za lishe, lakini swala la Utapiamlo bado ni changamoto kidogohasa kwenye kuwabaini hawa watoto wenye utapiamlo,

basi Watendaji wa Kata na vijiji, fanyeni vikao kuanzia ngazi za chini kabisa, mkiwashirikisha Vitongoji, ili iwe rahisi kuwabaini hawa watoto wenye Utapiamlo na waanze matubabu mapema" amesema bi. Kabojela.


Kikao cha tathimini ya lishe, kinalenga kuimarisha maswala mazima ya lishe, ili kujenga uelewa mkubwa kwa jamii na kuwa na jamii yenye afya bora ya akili na mwili.

Matangazo

  • Matokeo ya usajili wa Madereva. October 03, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • "Swala la Lishe sio la hiari, Utekelezaji wake ni wa lazima"- DC Frank Nkinda.

    July 30, 2025
  • MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA USHETU.

    July 27, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU YASHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA ZA AFYA.

    July 24, 2025
  • Bodi ya Afya ya Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu yazinduliwa.

    July 11, 2025
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0759888848

    Simu ya kiganjani: 0759888848

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa