Na. Emmanuel Shomary,
Ushetu DC,
Mei 20, 2025.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha, amefanya ziara ya kikazi kukagua maendeleo ya miradi itakayopitiwa na mbio za Mwenge wa Uhuru 2024/2025 katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu.
Ziara hiyo imefanyika leo Mei 20, 2025, ambapo jumla ya miradi saba (7), itakayopitiwa na mbio za mwenge wa Uhuru 2024/2025 yote ilifikiwa na ziara hiyo ya Mkuu wa Mkoa na kufanyiwa tathimini.
Miradi hiyo ya maendeleo inayotazamiwa kugharimu kiasi cha fedha Tsh. 3.34 bilioni ni pamoja na:
Akizungumza katika ziara hiyo, RC Macha amepongeza juhudi na maendeleo ya miradi hiyo ambayo kwa kiasi kikubwa imefikia hatua nzuri ya Ukamilishaji.
“Nawapongeza kwa kweli kwa juhudi mnaonesha, mpaka hatua mliofikia ninaimani mtakamilisha ndani ya muda muafaka na hapatakuwa na zile kazi za zimamoto, mimi na timu yangu tutaendelea kufuatilia ujenzi wa miradi hii mpaka hatua ya mwisho” alisema RC Macha.
Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kupokelewa Halmashauri ya Ushetu Augosti 4, 2025 katika viwanja vya shule ya Msingi Iramba kata ya Igwamanoni, Ukitokea Halmashauri ya Mji wa Kahama.
Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Anuani: S. L. P 50 Kahama
Simu: 0759888848
Simu ya kiganjani: 0759888848
Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz
Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa