Na Shomary Emmanuel.
Ushetu-kahama, Shinyanga.
June 17, 2022.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mh. Sophia Mjema ameongea na Wananchi wa Halmashauri ya Ushetu juu ya Kupanda bei kwa bidhaa mbalimbali, hasa bidhaa za mafuta.
Katika kikao hicho na Wananchi wa Ushetu, kilichofanyika leo Ijumaa, Juni 17,2022 kuanzia saa 9 alasili, katika viwanja vya Stendi ya Magari ya Nyamilangano, Makao makuu ya Halmashauri hiyo, Mheshimiwa Mjema, ameawataka Wananchi kuepuka kudanganywa na watu wenye nia ovu wanaolenga kuwagombanisha Wananchi na Serikali yao pendwa.
“Leo ndungu zangu nimekuja kusema na ninyi, juu ya kwanini vitu vimepanda bei, Ukweli ni kwamba, Uwepo wa Vita kati ya Urusi na Ukraine, umesababisha upungufu mkubwa sana wa Gesi na Ngano katika Nchi nyingi za Ulaya, kwani Urusi ndiye mzalishaji mkubwa wa Gesi, na Ukraine ndiye mzalishaji wa Ngano, hivyo kupigana kwa Mataifa hayo, kumepelekea upungufu mkubwa wa bidhaa hizo muhimu kwa Dunia nzima. Lakini pia msisahau kuwa uwepo wa UVIKO-19, wenzetu walijifungia kabisa, hivyo wenzetu walikuwa hawazalishi chochote, yote hayo yemepelekea uchumi kuyumba kwa Dunia nzima, hivyo wote wanaoisema vibaya Serikali ya Awamu ya Sita, Wapuuzeni tu”
Katika hatua nyingine, Mhe. Mjema, amewataka wananchi hao kuendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya Mama Samia Suruhu Hassan, kwani Mpaka sasa Serikali imetoa ruzuku ya Bilioni 100 kwenye Mafuta, ili kuzuia upandaji bei wa bidhaa hiyo.
“Ndugu zangu, Serikali ya Mama imetoa Ruzuku ya Bilioni 100 kwenye mafuta, na itaendelea kutoa hiyo Ruzuku kila mwezi, ili kukabiliana na kupanda bei kwa mafuta, na hivyo tutegemee mafuta kushuka bei kadri siku zinzvyokwenda.
Lakin pia ndugu zangu, Msisahau kuwa sasa hivi, watoto wetu wanasoma kuanzia Elimu ya Awali hadi Kitato cha Sita bure, jamani nani kama mama Samia?”
Mkuu huyo wa Mkoa, alimaliza kikao hicho, kwa kuwahamasisha Wananchi kuchanja Chanjo ya UVIKO-19, ambapo wananchi wengi walijitokeza kuchanjwa chanjo ya UVIKO-19 siku hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mh Sophia Mjema, akishuhudia Uchanjaji wa chanjo ya UVIKO-19 Nyamilangano Ushetu
Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Anuani: S. L. P 50 Kahama
Simu: 0759888848
Simu ya kiganjani: 0759888848
Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz
Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa