• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ushetu District Council
Ushetu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Maadili ya msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Strategic Plan
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Biashara na Fedha
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Takwimu,Mipango na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Land and Livestocks
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknoloji Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa ndani
    • Muundo wa halmashauri
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma
    • Bima ya Afya
    • Mitambo ya kutengenezea Barabara
    • Loan Services
    • Huduma za Afya
    • Education Services
    • Water Services
    • Huduma za Kilimo
    • Livestock Keeping Services
    • Huduma za Uvuvi
    • Human Resources Services
    • Huduma za Leseni za Biashara
    • Land Services
    • Forest Services
  • Madiwani
  • Miradi
    • Uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za maombi
    • Zabuni
    • Miongozo
    • Hotuba
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Uhifadhi wa picha
    • Video
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU YAPITISHA BAJETI YA SH.BILIONI 41.2 MWAKA WA FEDHA 2025/2026

Ilipo tumwa: February 5th, 2025

Na Emmanuel Shomary, Ushetu DC.

BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Ushetu Mkoani Shinyanga, limepitisha makadirio ya bajeti ya Sh.bilioni 41.2 kwa mwaka wa fedha ujao wa 2025/2026, huku likiwasisitiza wakulima wa mazao ya biashara kutotorosha mazao hayo ili kufikia lengo la makusanyo tarajiwa.

Aidha, limependekeza kupatiwa watumishi wapya 436 na watumishi 697 kupandishwa vyeo au madaraja na 19 kubadilishiwa madaraja yao.

Bajeti hiyo imepitishwa leo Feb 4,2025 katika kikao cha baraza la Madiwani la Halmashauri ya Ushetu na kuipongeza Serikali kwa kuendelea kuwapatia fedha za ukamilishaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo hususani ile iliyoanzishwa kwa nguvu za Wananchi kwenye sekta ya Afya na Elimu.

Akisoma makadirio hayo ya bajeti, Afisa Mipango wa Halmashauri hiyo bwana Shigela Ganja alisema, bajeti hiyo imeongezeka kulinganisha na mwaka unaendelea wa 2024/25 ambapo waliweka makadirio ya kukusanya na kutumia Sh.bilioni 35.5 ikiwemo mapato lindwa na yasiyolindwa.

Bwana Ganja alisema, mwaka wa fedha 2025/2026 wanatarajia kukusanya kiasi cha Sh.bilioni 41.2, huku mapato ya ndani yasiyolindwa ni Sh.bilioni 3.85, miradi ya maendeleo Sh.bilioni 1.5, matumizi menginenyo Sh.bilioni 2.3, Ruzuku ya Mishahara Sh.bilioni 25.6, Ruzuku ya Miradi Sh.bilioni 9.36, Ruzuku ya Serikali Sh.bilioni 4.6 pamoja na fedha kutoka kwa Wananchi Sh.bilioni 4.6.

Naye diwani wa viti maalumu wa kata ya Bulungwa bi. Ester Matone alisema,ili kufikia malengo hayo ni vema Halmashauri ikaendelea kuibua vyanzo vipya vya mapato na kuboresha vilivyopo kwani asilimia kubwa ya mapato yake yanatokana na zao la tumbaku kulinganisha na mazao mengine ya biashara.

Katika hatua nyingine, Diwani wa kata ya Nyamilangano, mh. Robert Mihayo alisema, utoroshaji wa mazao na kwenda kuuzwa kinyemela utasababisha kutokufikia malengo hivyo kila Diwani kwenye eneo lake ahakikishe analisimamia hili ili kufikia lengo la makusanyo kwa zaidi ya asilimia 100 kama ilivyotokea mwaka uliopita wa 2023/2024.

Matangazo

  • Matokeo ya usajili wa Madereva. October 03, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili August 22, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • USHETU KUANZA KUTEKELEZA MRADI WA REA NGAZI YA VITONGOJI 151.

    May 08, 2025
  • Habari Picha: Watumishi wa Halmashauri ya Ushetu wakumbushwa kuhusu Maadili katika utumishi wa Umma

    May 07, 2025
  • Tume ya Maadili kwa watumishi wa Umma wafanya kikao na watumishi wa makao makuu Halmashauri ya Ushetu

    May 05, 2025
  • Tangazo la uuzaji Viwanja vya Makazi na Viwanda vidogo.

    April 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Kilimo cha Korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Video

Viunganishi vya haraka

  • Kanuni za Utumishi wa Umma
  • Ufafanuzi wa Serikali juu ya Kukosekana kwa Mawasiliano ya simu katika Halmashauri
  • Facebook
  • Ramani ya Halmashauri

Viunganishi Mfanano

  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Ajira serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Halmashauri

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

    Anuani: S. L. P 50 Kahama

    Simu: 0759888848

    Simu ya kiganjani: 0759888848

    Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa