Banki ya NMB wilayani Kahama, imetoa msaada wa Vitanda vya wagonjwa nane (8), na mashuka ishirini na tano (25), katika Hospitali ya Wilaya ya Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, vyenye thamani ya jumla ya fedha Tsh. Milioni tano (5,000,000/=), Ikiwa ni Mchango wao katika kuboresha huduma za Afya kwa wakazi wa Ushetu.
Akizungumza katika hafla hiyo fupi iliyofanyika katika ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu, leo tarehe 6 Oktoba, 2020, Afisa rasilimali watu mkuu wa Banki ya NMB, ndugu Emmanuel Apolonari, amesema wao kama sehemu ya jamii na wadau wakubwa wa maendeleo, wanayo fahari kuendelea kuwa karibu Zaidi na jamii hasa kwa kuchangia maendeleo ya jamii hususani katika sekta ya afya.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Anamringa Macha, akipokea msaada huo, amewashukuru Banki ya NMB kwa msaada huo na kuwapongeza kwa mchango wao mkubwa kwa jamii, vile vile ameahidi kuendelea kushurikiana vyema na Banki ya NMB ili kuleta maendeleo yenye tija kwa wakazi wa Kahama na Watanzania wote kwa ujumla.
Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ushetu, ndugu Michael Augistine Matomora, amewashukuru Banki ya NMB kwa msaada huo, na kuahidi kuvitunza na kuhakikisha vinatumika katika matumizi sahihi ili kuwapatia huduma bora Wananchi wa Ushetu.
Hospitali ya Wilaya ya Ushetu, yenye Majengo saba (7), ambayo ni Jengo la Wagonjwa wa nje (OPD), Jengo la Utawala, jengo la dawa (Pharmacy), jengo la Kufulia (laundry), jengo la Mionzi, jengo la Maabara, na Jengo la Wazazi, ilianza kutoa huduma mnamo mwezi Juni 2020, ambapo takribani wagonjwa Elfu 80 wamepatiwa huduma katika Hospitali hiyo.
Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Anuani: S. L. P 50 Kahama
Simu: 0759888848
Simu ya kiganjani: 0759888848
Barua pepe: ded@ushetudc.go.tz Tovuti www.ushetudc.go.tz
Hati Miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu . Haki zote zimehifadhiwa